Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt as -ABNA- Sheikh Naeem Qasim: Israel leo iko dhaifu kuliko wakati wowote ule / Tuna hakika kwamba Iran chini ya uongozi wa Imam Khamenei bado itabaki imara na yenye heshima.
Katibu Mkuu wa Hezbollah Lebanon katika hafla ya kumbukumbu ya Shahidi Haj Ali Hassan Sulleh “Haj Malik”:
Hata kwa kuwa na rasilimali zote na msaada wa kimataifa, serikali ya Israel leo iko dhaifu kuliko wakati wowote ule na haijafanikiwa kutimiza malengo yake katika Lebanon, Gaza, Iran na Yemen.
Mapinduzi ya Iran hayakuwa ya Mashariki wala Magharibi; kwa miaka 47 bila kutegemea Mashariki au Magharibi, imebaki imara na yenye athari na imeendeleza upinzani (muqawama) katika eneo.
Jamhuri ya Kiislamu imefanikiwa katika mapambano yote, hasa dhidi ya uvamizi wa serikali ya Kizayuni, na tuna hakika kwamba chini ya uongozi wa Imam Khamenei bado itabaki imara, huru, thabiti na yenye heshima.
Your Comment